
19 December 2025
Tiba asilia zina nafasi muhimu katika kuimarisha mifumo ya afya duniani - WHO
Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu
About
Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya Duniani, WHO, linasema tiba asilia na tiba jadidifu zina nafasi muhimu katika mifumo ya afya duniani, hasa katika kinga, huduma za usaidizi wa magonjwa na kuongeza upatikanaji wa huduma za afya kwa jamii. Hayo yamebainishwa na Mkuu wa Kitengo cha Tiba Asilia, Jadidifu na Jumuishi cha WHO, Dkt. Sung Chol Kim, katika mahojiano maalum kando ya Mkutano wa Kimataifa wa Tiba Asilia unaoendelea huko New Delhi, India. Sabrina Saidi na taarifa zaidi..