Sadia Yahya, Mwanamke jasiri Sudan anayesongesha amani kwa kutegua mabomu ya ardhini
01 April 2026

Sadia Yahya, Mwanamke jasiri Sudan anayesongesha amani kwa kutegua mabomu ya ardhini

Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

About
Tarehe 4 mwezi Aprili mwaka huu ni siku ya kimataifa ya kuelimisha umma kuhusu mabomu ya  kutegwa ardhini ambayo yamekuwa ‘mwiba’ kwa wananchi walioko maeneo siyo tu ya vita hivi sasa bali pia yale ambamo mapigano yamemalizika lakini masalia ya mabomu yanaendelea kutesa wananchi. Nchini Sudan mwanamke mmoja anatekeleza kwa vitendo maudhui ya siku hii mwaka huu ambayo ni Wekeza kwenye amani, wekeza kwenye hatua dhidi ya mabomu ya kutegwa ardhini. Je anafanya nini? Ungana na Flora Nducha.