
12 November 2025
Ripoti mpya ya FAO/WFP yaonya muda unayoyoma kuzuia mamilioni kuingia kwenye njaa katika maeneo 16 hatarishi.
Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu
About
Ripoti mpya ya pamoja kutoka mashirika mawili ya Umoja wa Mataifa lile la Chakula na Kilimo Duniani (FAO) na la Mpango wa Chakula Duniani (WFP) inaonya kwamba uhaba mkubwa wa chakula unazidi kuongezeka katika maeneo 16 yenye njaa duniani, hali inayoweza kusababisha mamilioni zaidi ya watu kukumbwa na njaa kali au hatari ya kufikia kiwango cha baa la njaa. Anold Kayanda na maelezo zaidi.