
17 October 2025
Mradi wa UNDP na wadau wake wawasaidia wananchi kuondokana na umasikini
Habari za UN - Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu
About
Mradi wa kusaidia jamii kupambana na athari za mabadiliko ya tabianchi nchini Zambia mbali na kusaidia wananchi kwenye kilimo pia umewawezesha kiuchumi na kuwaondoa baadhi yao kwenye mstari wa umasikini. Mmoja wa walio utupa mkono umasikini ni Judith Mabeta aliyetoka kuishi nyumba ya udongo mpaka kuwa na nyumba ya kupangisha na sasa ni mama mwenye nyumba. Leah Mushi anatujuza zaidi.