Skip to content
Opens in a new window
About
Katika Jarida la Habari la Umoja wa Mataifa hii leo Flora Nduha anakuletea-Julien Harneis, Mratibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa Ebola  amesema  nchini DRC “Katika miezi mitatu iliyopita watu 2,500 wamekufa na nusu yao wamekufa katika kipindi cha siku tatu zilizopita na mlipuko unaendelea kusambaa zaidi, hivi sasa umesambaa katika eneo lenye ukubwa sawa na nchi ya Ufaransa.”-Hali ya ukosefu wa fedha ni mbaya pia nchini Somalia ambapo shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto, UNICEF limesema kuwa kupunguzwa kwa ufadhili wa kibinadamu nchini Somalia kumesababisha kufungwa kwa vituo 205 vya afya na lishe, huku watoto wanaougua utapiamlo mkali wakisafiri umbali mrefu kutafuta matibabu wakati mwingine wakifika hospitalini wakiwa katika hali mahututi.-Leo ni ni siku ya Kimataifa ya Kuwakumbuka na Kuwaenzi Waathirika wa Ugaidi Duniani, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres katika ujumbe wake kwa siku hii amezungumzia kaulimbiu ya mwaka huu inayosema “Uponyaji kupitia Kumbukumbu,” akasisitiza kuwa kuwakumbuka waathirika kunaweza kuwa njia ya kuelekea uponyaji na kuanza upya.-Na katika mada kwa kina leo tuko Uganda kwake manusura wa ugaidi Hassan Ndugwa akisimulia kilichomsibu 2010 na hatua alizochukua katka kupambana na itikadi kali na fikra potofu kuhusu ugaidi na kuudhibiti