About
Leo katika Jarida la Habari la Umoja wa Mataofa Flora Nducha anakuletea --Katika kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wahudumu wa Kibinadamu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres ametoa wito wa kuchukuliwa hatua za haraka kuwalinda wahudumu wa kibinadamu wanaotoa msaada wa kuokoa maisha katika maeneo yenye migogoro-Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya Kuratibu Masuala ya Kibinadamu na Misaada ya Dharura (OCHA) iliyotolewa leo katika kuadhimisha hii imeonya kwamba wahudumu 907 wa kibinadamu walikumbwa na vitendo vya ukatili mwaka jana, wakati wakitekeleza kazi zao za kuokoa maisha katika maeneo ya migogoro yanayozidi kuwa ya hatari.-Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa, Volker Türk, amesema ana wasiwasi kuhusu taarifa za kukamatwa na kuzuiliwa kwa wanachama wa vyama vya upinzani nchini Zambia kabla na baada ya uchaguzi mkuu uliofanyika Agosti 13 katika ncho hiyo ya barani Afrika.-Na katika mada kwa kina hii leo tunaye Muhudumu wa Kibinadamu Cedric Lusimba muuguzi aliyehudumu katika maeneo mbalimbali yenye mizozo