
28 July 2026
Fahamu kuhusu chanzo cha wimbi la joto kali linaloshuhudiwa Ulaya.
Mazingira Leo, Dunia Yako Kesho
About
Wimbi la joto kali limekumba bara la Ulaya kwa muda sasa, hali iliyosababisha viwango vya juu vya joto katika nchi kadhaa na kusababisha maelfu ya vifo.
Zaidi ya watu 300,000 wamehamishwa na angalau mtu mmoja alifariki dunia kutokana na moto wa nyika nchini Ufaransa na Uhispania, huku vikosi vya zimamoto vikipambana na mioto hiyo.
Leo katika uchambuzi wetu tunaungana na Daktari Joyce Kimutai, mwanasayansi wa tabia nchi kutoka mamlaka ya utabiri wa hali ya hewa nchini Kenya, anayetuelewesha zaidi kuhusu matukio haya na namna nchi zinaweza kuchukua tahadhari kuwalinda raia wake.